Aliyekuwa meneja wa Ommy Dimpoz afunguka haya

MUBENGA aliyekuwa meneja wa msanii, Ommy Dimpoz, ameibuka na kusema kuwa tangu aache kumsimamia msanii huyo, amepoteza dira kimuziki, ndiyo maana hatoi nyimbo kwa wakati.

“Tukizungumza kwa namna ambavyo mimi nimefanya kazi na Ommy, vitu vingi vinavyomtokea sasahivi sielewi hata mimi nashangaa, kwa sababu ukiangalia hata kwenye gemu yetu hafanyi vizuri tena, sijui anakosea wapi, hata kazi zake hazina ubora na hazitoki kwa wakati.

“Nakumbuka wakati tunafanya kazi kuanzia Nai Nai, Baadaye, Ndagushima, Me and You, Tupogo, Wanjera ni nyimbo ambazo zilikuwa zinatoka kwa wakati, na mapokezi yake yalikuwa ni makubwa sana.

“Sijui labda yeye mwenyewe anajiona wapi, lakini mimi simuoni pale ambapo nilikuwa nimemfikisha,” amesema Mubenga.

Baada ya kutemana na Mubenga, Ommy Dimpoz kwa sasa yupo chini ya menejimenti ya Rockstar, ambayo ndiyo inayomsimamia Ali Kiba.  

Comments

Popular posts from this blog

Tembo wapiga kambi kata ya Mkoka, wamjeruhi mtu na kula mzao mashambani

Sugu awashangaa wanachama wa CCM

Shamsa Ford ampa somo Shilole kuhusu ndoa