Pata habari za uhakika na zilizo fanyiwa uchunguzi wa hali ya juu.
Profesa Kitila Mkumbo ajiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM)
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Profesa Kitila Mkumbo amejiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM), taarifa ya
Prof. Mkumbo kujiunga CCM imetolewa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Singida, Martha Mlata.
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kumjia juu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai na kusema kuwa anamsikitika sana kama haoni jeshi heshima ya Bunge inavyoshuka. Zitto Kabwe amesema hayo leo kupitia mitandao yake ya kijamii baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kuagiza na kuwataka wabunge Zitto Kabwe pamoja na Saed Kubenea wa Ubungo kufika kwenye Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge kuhojiwa kutokana na kauli zao ambazo wamezitoa hivi karibuni. Kufuatia wito huo Zitto Kabwe amesema yeye atafika kwenye kamati hiyo ya maadili na Madaraka ya Bunge kama ambavyo Spika wa Bunge Job Ndugai ameagiza na kusema kuwa spika huyo kama angeweza kujua nguvu yake wala asingehaika na wabunge ambao wanakosoa kwa staha. "Spika Ndugai anajua ninavyomheshimu kama imefikia haoni heshima ya Bunge inavyoporomoka namsikitikia. Nitakwenda Kamati ya Maadili, Ndugai amekuwa Spika wa kwanza katika historia ya nchi yetu kus...
Milango ya ustaa inazidi kufunguliwa kwa Diamond Platnumz. Msanii huyo kutoka WCB ameonekana kuanza kuwateka mastaa wakubwa Marekani. Baada ya Dj Khaled kumfollow na rapper Rick Ross kumpost hitmaker huyo wa Eneka kwenye mtandao wa Instagram, Swizz Beatz na yeye ameamua kufuata nyayo kama hizo. Swizz ameonekana katika kipande ha video akimtaja Diamond. Hata hivyo haikuishia hapo producer huyo ambaye pia ni mume wa msanii Alicia Keys ame-comment katika video hiyo ambayo Diamond ameipost katika mtandao huo. “@diamondplatnumz Bless up Kingππππππππππππ,” ameandika Beatz katika video hiyo
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amewashangaa wananchama wa CCM waliolipigia hesabu jimbo hilo, akidai kuwa wanajisumbua kwa sababu walishapoteana tangu mwaka 2010. Akizungumza leo Desemba 20 katika mahojiano maalum na MCL Digital, Sugu amesema viongozi wa CCM wanaojipambanua kutaka chama hicho kishinde majimbo ya upinzani, ikiwa ni pamoja na kuongoza halmashauri wanapoteza muda. “Wanataka kurudisha jiji la Mbeya mikononi mwao sambamba na kata zote ambazo tulishinda katika uchaguzi uliopita. Wanajisumbua,” amesema. Sugu alikuwa akimjibu Mwenyekiti mpya wa CCM mkoani Mbeya, Jacob Mwakasole ambaye mara baada ya ushindi huo ameshangazwa na upinzani mkali uliopo katika jiji hilo. Mwakasole amesema mkoa huo unazo changamoto nyingi za kisiasa na makundi ndani ya CCM, kuwataka wanachama kushikamana kuzishughulikia ili kurudisha nguvu ya chama hicho ili kulirejesha jimbo hilo mikononi mwa CCM. “Ni wazi CCM wamepaniki na k...
Comments
Post a Comment