Utapeli wa bomba Tanga, Wananchi warubuniwa kwa ahadi ya kupata ajira

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza kwenye baraza la madiwani wa jiji hilo kufuatia taarifa za kuzuka kwa magenge ya utapeli yaliyojipachika uwakala wa kusimamia mchakato wa ajira kutoka katika mradi huo.
Amesema ajira za Serikali zinatangazwa kupitia utaratibu wa wazi ambao upo kisheria bila ya kupitia kwa uwakala.
Kwa upande wake meya wa jiji la Tanga Mhina Mustafa (Selebos ) amesema halmashauri imekamilisha upimaji wa viwanja 4000 katika maeneo ya amboni ambavyo vitatangzwa hivi karibuni na kuwataka wananchi kujitokeza kuomba.
Aidha amewaonya wananchi wanaonunua viwanja kiholela na kujenga bila kibali cha jiji kuacha mara moja ili kuepuka kubomolewa nyumba zao.
Comments
Post a Comment