Posts

Showing posts from December, 2017

Sugu awashangaa wanachama wa CCM

Image
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema),  Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amewashangaa wananchama wa CCM waliolipigia hesabu jimbo hilo, akidai kuwa wanajisumbua kwa sababu walishapoteana tangu mwaka 2010. Akizungumza leo Desemba 20 katika mahojiano maalum na MCL Digital, Sugu amesema viongozi wa CCM wanaojipambanua kutaka chama hicho kishinde majimbo ya upinzani, ikiwa ni pamoja na kuongoza halmashauri wanapoteza muda. “Wanataka kurudisha jiji la Mbeya mikononi mwao sambamba na kata zote ambazo tulishinda katika uchaguzi uliopita. Wanajisumbua,” amesema. Sugu alikuwa akimjibu Mwenyekiti mpya wa CCM mkoani Mbeya,  Jacob Mwakasole ambaye mara baada ya ushindi huo ameshangazwa na upinzani mkali uliopo katika jiji hilo. Mwakasole amesema  mkoa huo unazo changamoto nyingi za kisiasa na makundi ndani ya CCM, kuwataka wanachama  kushikamana kuzishughulikia ili kurudisha nguvu ya chama hicho ili kulirejesha jimbo hilo mikononi mwa CCM.  “Ni wazi CCM wamepaniki na k...

Wanaohubri kwenye mabasi kukiona cha moto

Image
Baraza la Ushauri wa watumiaji wa huduma za safiri wa nchi kavu na majini, SumatraCCC limekitaka chama cha wamiliki wa mabasi nchini TABOA na washirika wao kuhakikisha wanasimamia vyema suala la baadhi ya watu kugeuza magari kuwa sehemu ya mahubiri suala mabalo limekuwa likilalamikiwa kila mara. Akizungumza na waandishi na habari, Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri watumiaji Sumatra, Oscar Kikoyo, alisema kuwa mabasi yatakayo kiuka kanuni hiyo faini zinawanyemelea. “Tuna kanuni mpya za mwaka 2017 ya usafiri na hii kanuni ilipigiwa kelele sana, lakini kulingana na kanuni ya 27(b) kipengele cha 3 mabadi si sehemu ya gulio wala mabasi si msikiti wala makanisa kwenda kuhubiri dini kule ndani, kufanya biashara pamoja ni miziki na filamu ambazo azikidhi viwango na desturi za Kiafrika, kama kuna mabasi yanakiuka hii kanuni wajue hii faini inawanyemelea ,” alisema Kikoyo

Mourinho kuiongoza United dhidi ya Bristol leo

Image
Ni miaka 37 sasa imepita tangu mara ya mwisho kwa Bristol City kukutana na Manchester United katika mashindano na hii leo kwa mara nyingine tena Bristol watawakaribisha United katika michuano ya Crabao Cup. Katika mechi ya mwisho mwaka 1980 Manchester United waliichapa Bristol kwa mabao 4 kwa 0 huku mabao ya United kwa wakati huo yakifungwa na Joe Jordan(2),Sammy McLloy na bao la kujifunga la Geoff Mereck. Bristol sio wa kuchukulia poa hata kidogo kwani wana timu inayoonekana kujituma sana na ndio maana katika robo fainali mbili zilizopita walizocheza walishinda zote mbili, moja na Fulham na nyingine na Bradford. Hii ni mara ya saba kwa United kufika robo fainali ya michuano hii katika mara 10 ambazo wameshiriki, na katika robo fainali sita zilizopita Manchester United wamefudhu kwenda nusu fainali mara nne. Haitakuwa ajabu sana kwa United kutolewa na Bristol kwani United wameshatolewa mara 3 na timu ambazo hazipo ligi kuu Crystal Palace 2011-2012, Mk Dons 201...

Shamsa Ford ampa somo Shilole kuhusu ndoa

Image
STAA wa Filamu nchini, Shamsa Ford amefungukia uamuzi wa msanii mwenzake wa Muziki, Zuwena Mohammed maarufu kama Shilole kwa kuamua kufunga ndoa tena ya Kidini na mpenzi wake, Uchebe ndoa iliyoshuhudiwa hivi karibuni na kutikisa kwenye mitandao na vyombo vya habari huku ikiwaacha midomo wazi kwa wale walidhani kuwa angerudiana na mpenzi wake wa zamani, Nuh Mziwanda. Shamsa ambaye pia alifunga ndoa mwaka huu na mpenzi wake, Chidi Mapenzi ametumia ukurasa wake wa Instagram kumsihi Shilole atulie, aweke umaarufu pembeni, aitunze ndoa yake na hatimaye atafaidi matunda ya ndoa iliyo bora. Shamsa ameandika; “Hongera sana mamy. Umefanya maamuzi sahihi ya kumpendeza Mwenyezi Mungu.Cha muhimu uwe mke bora wa Kitanzania kwa mumeo na ustar uweke pembeni. “Mumuweke Mungu mbele, uvumilivu na kuheshimiana inshaallah mtazikana.Karibu kwenye Chama mama….Sasa nyie mnao subili matajiri wawaoe wakati hao matajiri wana wake zao wameanza nao moja mtasubili sana mpaka uso uote sugu.Uzur...

Hiki ndicho kilipelekea Mourinho na Arteta kupigwa chupa, Mourinho ndio chanzo

Image
Haikuwa rahisi hata kidogo kwa Derby kubwa na ngumu kama ya Manchester kuisha hivi hivi bila kuwa na habari kubwa, na matokeo ya mechi ilikuwa habari iliyotarajiwa kwani mpira wowote lazima kuwe na matokeo. Habari isiyotarajiwa ni tukio lililotokea baada ya mchezo huo ambapo inadaiwa kocha Jose Mourinho alikuwa chanzo cha fujo kubwa iliyotokea katila vyumba vya kubadilishia nguo baada ya mchezo huo. Inadaiwa kwamba wachezaji wa Manchester City walikuwa wakishangilia sana katika vyumba vya kubadilishia nguo huku wakiwa wamefungulia sauti ya mziki kubwa sana kiasi cha kuwasumbua wengine. Jose Mourinho hakufurahia jambo hilo na aliamua kwenda kuwaambia wapunguze sauti, lakini wakati Mou akiwaambia hivyo kulitokea hali ya majibizano kati ya wachezaji wa Citu wakiongozwa na golikipa Ederson na kocha huyo wa United. Inadaiwa Ederson alikuwa akibishana na Mourinho na wakati wakiendelea kubishana ndipo kulirushwa kopo la maji ambalo halikumpata vizuri Mourinho na baadae watu...

Handeni: Wauzaji wa nyama wagoma kufungua maduka ya kuuzia bidhaa hiyo.

Image
Wauzaji wa nyama pamoja na wachinjaji wanaofanya shughuli zao kwenye machinjio yaliopo wilayani Handeni mkoani Tanga wameendesha mgomo wa kutokuchinja na kuuza nyama mpaka pale viongozi wa halmashauri watakaposikiliza kero zao na kuzitatua ikiwemo ya kulazimiswa kutumia gari maalum la kusambaza nyama hali ambayo wamesema kuwa hawakushirikiswa ipasavyo kwenye swala hilo. Kamera ya ITV imefika machinjio ya wilaya na kukuta yakiwa meupe bila kuwepo dalili ya kupatikana huduma hiyo na ilifanikiwa kuongea na mwenyekiti wao na hapa anaelezea sababu. Hata hivyo mkurugenzi wa halmashauri ya mji alifika machinjioni hapo na kukiri kuwa kweli ushirikishwaji haukufanyika huku wafanya biashara hao wakimkataa daktari wa machinchio hayo mbele ya mkurugenzi.

Steve Nyerere amjia juu Polepole kuhusu Wema Sepetu

Image
HABARI inayobamba mitandaoni na kwenye vyombo vya ahabri kuanzia jana jioni ni kuhusu Malkia wa Filamu Bongo, Wema Sepetu kuhama Chadema na kutangaza kurudi kwenye Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo uamuzi huo umetolewa ufafanuzi na Katibu wa Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akisema CCM haina taarifa za Wema kwani hajafuata taratibu kuanzia kwenye shina la chama na si kupitia mitandaoni. “Chama chetu sio Daladala mtu anaweza kupanda na kushuka wakati wowote, ni heri akabaki hukohuko ama akaanzie kule ambako alichukulia kadi yetu,” aliandika Polepole. Kauli hiyo imemuibua Staa wa Filamu aliyekuwa rafiki wa karibu wa Wema kabla hajahamia Chadema, Steve Nyerere ambaye amemtolea povu Polepole na kuijibu kauli yake hiyo akiandika; “Hiki chama hujakiunda wewe wala kukianzisha wewe, umekikuta kama tulivyokikuta wote, kina waasisi wenye uchungu nacho na wako kimya. “Wewe ni nani ukatishe watu moyo kukitumikia kama vile ndio unakimiliki, tulia polepole chama cha wote hiki, u...

Mama Wema afunguka, adai kadhalilishwa na mwanawe

Image
Mama mzazi wa msanii Wema Sepetu ambaye hapo jana ametangaza kurudi CCM, Bi, Mariam Sepetu, amesema kitendo cha Wema kurudi CCM bila kumuomba ushauri ni kitu ambacho kimemdhalilisha kama mzazi. Mama Wema ameyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kufuatia kitendo cha Mawanaye kurudi CCM, huku lawama nyingi zikiwa zinamuelekea yeye kama mzazi kwa kutomshauri vema binti yake. Akiendelea kuzungumzia suala hilo, mama Wema amesema watu wanaomshauri Wema kama wazazi wake si watu wazuri akimtaja Steve Nyerere, huku akisema hawana mapenzi ya kweli na Wema kwani alipopata matatizo walimkimbia, na badala yake CHADEMA ndio waliokuwa wakihangaika naye. "Nasema haya kuhusiana na Steve, Wema alipopata matatizo hakuweza kutokea central kumuona Wema, leo anashangilia Wema kurudi CCM, lakini akumbuke mimi nitabaki kuwa mzazi, CHADEMA walipoona nataabika nahangaika, waliweza kuja mpaka nyumbani kwangu, kuja kutoa pole, wamemsaidia Wema, napenda kusema CHADEMA ni fami...